Wednesday, 15 August 2018

KILA ALIYE SIMAMA ALIANGUKA



                              
                         KILA ALIYE SIMAMA ALIANGUKA
Kuteleza si kuanguka usemi huu ulisemwa na wahenga wakimanisha kuwa sio kila kujikwaa kunasababisha kuanguka , unaweza ukateleza katika safari na usianguke ila hauwezi kuanguka usipo teleza .Moja kati ya mambo ambayo ni kikwazo kikubwa kwa watu wengi katika safari ya kuelekea mafanikio  ni kuanguka  kwa mambo muhimu  wanayokuwa wanategemea  na inapokuwa  imetokea tayari mtu ambaye alikuwa  ameweka imani yake katika jambo hilo ambayo linaweza kuwa la kisiasa, kiuchumi , kielimu, kiroho ,kimahusiano basi mtu huyo hupata anguko kuu linalo anza moyoni . inawezekana  unaposoma makala hii tayari kuna mambo yameshakuangusha kiasi cha kuona kuwa hauwezi kuinuka kabisa .Lakini leo napenda nikwambie kuwa kila aliye simama alianguka .Ukipata mda wa kufatilia maisha yao utaona wazi kuwa hakika walianguka anguko ambalo haikuwa rahisi kwao kuinuka tena ,tunaona mfano kwa aliyewahi kuwa raisi wa Marekani Abraham  Lincoln alianguka zaidi ya mara arobainina saba(47) katika safari yake ya kuelekea mafanikio bila kufanikiwa na katika anguko hilo aliaminikuwa siku moja atainuka na kufika katika kilele cha mafanikio yake .Haikuwa rahisi kwa Lincolin kuinuka unaweza ukajiuliza maswali kadha wa kadha nini kilimfanya Lincolin anguke mara safari zote  hizo , unaweza usipate majibu sahihi ila nataka uone kuwa safari zote hizo ni matokeo ya kuwa kila alipo anguka hakuamini kuwa ndiyo mwisho wa safari yake ,alicho kiamini nikuwa safari yake itafika mwisho hadi pale atakapo fikia kila anachokiamini katika ndoto zake.Hebu jiulize ni mara ngapi umeanguka katika safari yako ya mafanikio ? Inawezekana umeanguka mara moja au zaidi ya mara moja jibu unalo wewe ,pamoja na hayo inawezeka kana mpaka sasa tayari pamoja na kuanguka mara chache hizo ulicho kwisha kuanguka na umeona kuwa tayari ni mwisho wako wa safari ya kuelekea mafaniko.Anza leo kuweka imani hii kuwa kila haijalishi umekwisha kuanguka mara ngapi katika Kilimo , Siasa , Mahusiano , Elimu, Biashara ,Unasanii wa nyimbo za injiri au mziki wa kidunia, Uigizaji Michezo mbalimbali leo unaposoma makala hii anza kuweka imani na kujiambia kuwa    lazima nifike mwisho wa kilele cha ndoto zangu.
Katika kipindi hiki cha kuanguka katika safari ya kuelekea kwenye kilele cha mafanikio kuna mambo muhimu lazima uyajua na kuyaishi ,leo napenda nikwambie mambo muhimu mawili ya kujua na kuyaishi
Usimulaumu mtu yeyote
Lawama ni moja ya jambo ambalo linakwamisha watu wengi sana katika kufika kilele cha mafanikio yao kutokana na kuwa lawama huamsha hisia na maumivu makubwa mno ambayo huongeza kiwango cha kukata tamaa.Pia lawama husiba nafasi ya kuziba fursa ya kuona milango mingine ya  ambayo ingesaidia katika kutatua changamoto zinazofanya mtu aanguke tena lawama  huondoa  ujasiri kwa mtu kuamini  kuwa kuanguka ni sehemu ya safari ya mafanikio ,lawama huondoa nguvu za mtu kuinuka tena na kuendelea katika safari ya mafanikio ya kufikia ndoto zake.Hivyo inawezekana  tayari  umeshaangushwa mara nyingi  na watu  tena wakati mwingine waliokuangusha ni  Ndugu zako wa karibu ambao uliwaamini sana kuwa wangekusaidia

kufika katika kilele cha safari ya mafanikio yako  lakini leo upo hivyo ulivyo  kwa sababu ya maumivu yaliyotokana na kulaumu watu uliowategemea ,haujachelewa katika kipindi hiki usilaumu mtu yeyote badala yake pata mda mwingi wa kutafakari sana mambo kadha wa kadha ambayo yamechangia kuangua katika jambo ulilo litegemea kasha anza kuangalia na wengine mfano kama Abrahamu Lincolin ambaye pamoja na kuanguka mara arobaini na sabu (47) bado akafanikiwa  na kufikia katika ndoto  yake ya kuwa raisi wa Marekani.Tabia ya kulaumu kumewafanya watu wengi sana kufa na ndoto zao kwa sababu walipo angushwa na watu wao wa  karibu walianza kuwalaumu na kupoteza tumaini kabisa kwa kuwaza kuwa haiwezekani tena kwa wao kuinuka na kufika katika kilele cha mafanikio yao.
Amini ndoto yako
Kila msafiri hupanga safari anayojua mwisho wake  na atashangaa  sana asipofika mwisho wa safari yake anapajua anapotakiwa kwenda  ila hatashangaa  akifika  kwa kuwa alijua mwisho wa safari yao.Ndvyo ilivyo hata kwako wewew unayesoma makala hii  najua unayo ndoto kubwa sana ambayo unaiamini  kuwa siku moja  itatokea maishani mwako .Hijalishi utaangushwa marangapi pengine na Ndugu zako au watu wako wa karibu wewe amnini ndoto zako tu ,Abraham Lincolini  aliamini katika ndoto zake kuwa iposiku ataifikia ndiyo maana hata alipo anguka zaidi ya mara 47 hakukata tama  kwani angeshangaa kama asingekuwa raisi wa taifa la marekani  ila hakushangaa  kwa kuwa  aliamini hivyo kuwa  ndoto zake zingetimia za kuwa raisi wa Marekani
Hitimisho
Usihesabu juu ya mara ngapi  umeangushwa bali  fikiria ndoto zako zitatimia  lini  na  kadri  utakavyo kuwa unafikiri mara kwa mara  utajiongezea nafasi kubwa ya   kuwa kufanikiwa kwa kuwa utaona mlango wa kuku fanikisha katka ndoto zako.


Monday, 17 April 2017

MAMBO MKUU MATATU YANAYO CHELEWESHA MTU KUFANIKIWA KIUCHUMI

MAMBO  3 YANAYO CHELEWESHA MTU KUFANIKIWA KIUCHUMI


Mpendwa msomaji wangu leo napenda tujifunze juu ya mambo ambayo husababisha mtu kuchelewa kupata mafanikio ya kimaisha .
Kila binadamu aliyeumbwa na Mungu hutamani sana kuwa na mafaniko makubwa sana kiroho na kiuchumi .Katika jitihada za kufikia mafanikio hayo kila mtu huomba Mungu kulingana na imani yake ,lakini pamoja na jitihada hizo za kumuomba Mungu ili kufanikiwa kiuchumi yapo mambo makuu matatu yanayo chelewesha  mafanikio  yako  katika misingi sahihi

(1) KUTOKUJUA KUSUDI ULILOITIWA KUTIMIZA
Ni mpango wa mungu kumuumba mwanadamu ili alitimize kusudi lake ,lakini watu wengi sana wapo hapa duniani na hawajui kusudi lililo waleta kulitimiza hapa duniani hali ambayo inapelekea kuishi nje ya mpango wa mungu na kusababisha kuchelewa au kushindwa kabisa kupata kile wanacho sitahili kupata .Mungu anakujua hata kabla hajakuumba ,ila anachotaka kwako ni wewe kumuuliza  Mungu ujue kusudi alilokuitia ili uweze kulitimiza ,mfano Yeremia aliitwa kuwa nabii (Yermia 1:5) ukitambua kusudi la wewe kuwepo hapa duniani itakuwa rahisi kufikia mafanikio yako haraka

(2) KUTOKUSIKIA MAAGIZO YA MUNGU
Ni mpango wa mungu kwa mwanadamu kufanikiwa katika mambo yote  ila usipo  sikiliza maagizo ambayo mungu anakuagiza kufanya kila siku utachelewa kupata mafanikio kwani kila utakalo lifanya litakuwa nje ya mapango wa mungu .Mungu ame ahidi kukupa mambo mengi sana kama uko tayari kuyasikiliza  na kuyafanyia kazi maagizo akuamuruyo kuyafanya kila siku  utapata baraka nyingi sana ambazo  zitakupeleka katika mafanikio ya kimwili na kiuchumi kataika misingi sahihi.Mungu ameahidi kukupa baraka nyingi sana kama uko tayari kusikiliza katika maagizo akuagizayo kila siku
 (Kumb 28:1-13)

(3) MASHAKA NA KUTOKUAMINI  JUU  YA VITU  UVIOMBAVYO  KWA  MUNGU WAKO
Watu wengi wanaomba sana kwa mda mrefu ili waweze kufanikiwa ili kutokana na mashaka na kutokuamini juu ya kila wakiombacho huchelewa kufikia mafanikio .Pamoja na kuomba mungu wako kulingana na imani yako ondoa mashaka na weka imani juu ya kile ukiombacho  utakipa (Yakobo 1:6-8)

Ninakushukuru sana kwa kutenga mda wa kusoma maada hii .Mungu akubariki 
Mada ijayo tutajifunza juu ya namna ya kujua kusudi ulilo itiwa kulitimiza 

Ni mimi mpendwa wako Novath Kasiano
kwa masiliano zaidi nipigie  kwa NO:0762 736 689/ 0753 485 656/0786 102 869
na barua pepe ni novathkasiano@gmail.com


Friday, 7 April 2017

NGUVU YA NIDHAMU KATIKA KUFIKIA MAFANIKIO


M
                          NGUVU YA NIDHAMU KATIKA KUFIKIA MAFANIKIO

Nidhamu  ndiyo chanzo cha mafaniko yoyote ambyo mtu anatamani kuyafikia katika kutimiza ndoto zake .Mafanikio ya mtu hupimwa pindi anapokuwa ameanza kuishi ndoto zake ,mafanikio ambayo mtu anatafuta katika maisha ya kila siku  yamegawanyika katika makundi makuu matatu
1 Mafanikio kiuchumi.
Hili ni kundi mojawapolakupima mafaniko ya mtu , kwani ni ukweli usiopingika kuwa watu wengi hutamani sana kufanikiwa katika eneo la uchumi , kwa sababu mafanikio ya kiuchumi hufungua milango ya mafanikio mengine .Watu walio fanikiwa kiuchumi ndio pia wana nafasi ya kufikia mafanikio ya makundi mengine kwani mafanikio haya pia huleta pesa za kutosha ambazo ndo hizo zinazo leta jawabu la mambo yote( MUHUBIRI 10:19C)

2 Mafanikio kisiasa
Siasa ndiyo ambayo hutawala sana karibu mifumo yote ya kiutawala ambapo utawala uaotawala eneo flani ndio unao amua ana ya  mfumo wa kiuchumi wa eneo hilo .Wanasiasa wengi hutamani sana kufanikiwa katika eneo hili .Jambo moja muhimu ni kujua umuhimu wa kuwa na nidhamu ya kufatilia sana mambo ya husuyo siasa ili kupata taaifa nyingi na maarifa mengi ambayo yatakusaidia katika kufikia mafanikio kwenye eneo hili la siasa

Kama unataka ufanikiwe katika siasa anza leo kuweka nidhamu ya kufatilia sana maswala ya siasa ili kupata taarifa sahihi na maarifa mengi na utaona matokeo yatakayo kufikisha kwenye eneo hilisiasa ili kupata taaifa nyingi na maarifa mengi ambayo yatakusaidia katika kufikia mafanikio kwenye eneo hili la siasa


3 Mafanikio kiroho
Ni wazi kuwa kila mtu kutokana na imani yake katika dini yake anatamani  sana kukuwa kiimani (kiroho) na kukuwa huko kiimani(kiroho) hapo tunasema mtu huyu amefanikiwa
Licha ya mafanikio kugawanyika katika makundi makuu matatu nayo hutegemea mambo makuu matatu ambayo ni fedha , mda  na mipango mizuri
Leo napenda tuangalie nguvu ya nidhamu katika fedha , mda na mipango mizuri ili kufikia mafanikio  hayo

1 Nidhamu ya fedha
Fedha huleta jawabu la mabo yote (MUHUBIRI10:19C) ,ikiwa na maana kuwa fedha ndiyo nguzo ya kwanza  katika kuleta mafanikio makubwa kiuchumi , kisiasa na kiroho ikiwa tu utakuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha .Nidhamu nzuri ya fedha husaidia katika kutekekeza mipango mizuri  ili kufikia mafanikio . Mafanikio yako hayategemei wingi wala uchache wa fedha ulizo nazo bali hutegemea nidhamu katika matumizi ya kiasi cha fedha katika kuleta mafanikio .

2  Nidhamu katika matumizi ya mda
Waswahili husema mda ni mali lakini kama haujui dhana halisi ya usemi huu  utaona kama ni jambo la kawaida sana ,hata mimi kabla sijaelewa dhana ya msemo huu nilijua kuwa kitu cha msingi sana katika maisha ni kuweka nidhamu katika fedha na sio matumizi mazuri ya mda  ,lakini baada ya kujua thamani ya mda ningependa nukufahamishe nguvu ya nidhamu katika matumizi ya mda .Mungu ametupa mda wa masaa ishirini na nne (24) kila siku sawa na masaa elfu saba mia nane na sitini(7860) kwa mwaka mzima ila ni mda huohuo wapo watu matajili na watu masikini  sana ,hivi umewahi kujiuliza kwa nini watu wengi sio matajili au kwa nini watu wengi hawana mafanikio mkubwa  lakini kuna wachache wamefanikiwa sana wakati wote hao wana mda sawa kwa kila siku,siri kubwa ni kwenye nidhamu ya matumizi ya mda .Mafanikio yako yanategemea sana jinsi unavyo tumia mda wako vizuri katika kutimiza malengo yako.
 Anza leo kuwa na nidhamu katika matumizi ya mda katika mambo uliyopanga kuyafanya utaona matokeo

Nidhamu katika kutekeleza mipango yako
Kupanga ni kuchagua ,usemi huu umezoeleka sana masikioni mwa watu wengi sana ,lakini leo napenda nikwambie nguvu ya nidhamu katika kutekeleza mipango inavyoleta mafanikio haraka,katika mpango wowote katika kuleta mafanikio  kuna vitu vinaitwa vipaombele na maana ya vipaombele ni vitu vya msingi katika mpango wowote ambapo mafanikio ya lengo lolote hutegemea kukamilika au utekelezaji mzuri wa hivyo vipaumbele .ni wazi kuwa kila mtu ana mipango mbalimbali ya kutekeleza ili kufika mafanikio anayotaka na katika mipango hiyo kuna mikakati mbalimbali ya kutekeleza ili kufikia malengo hayo ,kitu cha muhimu kujua ili uweze kufanikiwa katika kufikia malengo yako ni kuweka nidhamu katika kutekeleza vipaumbele vitakavyo fanikisha mpango wako ,kwa maneno mingine ni kusema usikubali kutekeleza kipaumbele hata kimoja kwani kushindwa kukamilika kwa kipaumbele kimoja husababisha kushindwa kwa kukamilika mpango mzima ambao ndio ungekupelekea kufikia malengo yako . kinachotofautisha kati ya waliofanikiwa na amabao hawajafanikiwa ni nidhamu katika kutekeleza vipaumbele vya mpango wa kufikia malengo
Anza leo kuhakikisha unaweka nidhamu katika kuteleza vipaombele vya mpango uliojiwekea utaona matokeo mazuri sana katika kufikia malengo yako

Hitimisho 
Watu wote duniani walio fikia malengo yao walikuwa na nidhamu katika matumizi ya mda,fedha na mipango hata wewe haujachelewa anza leo kuwa na nidhamu katika matumizi ya mda ,fedha na mipango nakuhakikishia kuwa utafikia malengo yako